Alhamisi, 18 Desemba 2014

JE WAIJUA MBEGU YA ZAO LA PARETO AINA YA MACHIPUKIZI?



Mbegu aina ya machipukizi hutokana na shina la zamani la pareto, shina hilo hung’olewa na baadaye huchanwa chanwa katika mche
moja moja na pasipo kuumiza mche.
 Ukisha andaa mbegu zoezi la kuandaa shamba na upandaji, linafuata. Shamba lilimwe vizuri kwa
kwa kuondoa magugu masumbufu kama Sangari. Matuta yenye sentimeta 60 toka tuta hadi tuta yaandaliwe.

Faida ya kutumia machipukizi ni
1. Mimea karibu yote hutoa maua kwa wakati mmoja
2. Ina kiwango cha juu cha sumu kwa kuwa mimea yote hufanana
3. Kipato cha maua makavu katika hekta ni kikubwa

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni